• This is default featured slide 1 title

    Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

  • This is default featured slide 2 title

    Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

  • This is default featured slide 3 title

    Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

  • This is default featured slide 4 title

    Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

  • This is default featured slide 5 title

    Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Gwajima afutiwa kesi ya Pengo

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam imefuta kesi ya Askofu Mkuu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima ya kutoa lugha ya matusi dhidi ya Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo.

Sababu ya kufutwa kesi hiyo ni Serikali kushindwa kupeleka mashahidi mahakamani kwa wakati.

Kesi hiyo ilifutwa jana na Hakimu Mkazi Mkuu Mfawidhi, Cyprian Mkeha kesi hiyo ilipokuja kusikilizwa mashahidi wa upande wa Jamhuri.

Mkeha aliifuta kesi hiyo chini ya Kifungu cha 225 cha Mwenendo wa Makosa ya Jinai (CPA), kwa sababu katika miezi 14 ya kesi hiyo kusikilizwa mahakamani hapo, upande wa Jamhuri ulipeleka shahidi mmoja.

Hakimu alifikia uamuzi huo, baada ya Wakili wa Serikali Mwandamizi, Joseph Maugo kuiambia Mahakama kuwa kesi hiyo ilikuja kusikilizwa, lakini hawakuwa na shahidi, hivyo kuomba ahirisho lingine.

Awali, Askofu Gwajima alikanusha tuhuma za kumtukana Askofu Pengo, baada ya kusomewa maelezo ya awali (PH) na Wakili wa Serikali, Maugo.

Maugo aliiambia Mahakama kuwa katika tarehe isiyojulikana kati ya Machi 16 na 25, Askofu Gwajima alitoa mahubiri kwa wafuasi wake, kwenye viwanja vya Tanganyika Packers, Kawe, Dar es Salaam.

Alidai wakati akitoa mahubiri hayo alitoa maneno ya matusi na ya kumfadhaisha Askofu Pengo, kuwa yeye ni mtoto, mpuuzi na mwenye akili ndogo sijui amekula nini? Mpuuzi yule, mjinga yule na yeye kuwa anaitwa Askofu Gwajima.

Wakili huyo alibainisha kuwa Askofu Gwajima wakati anatoa maneno hayo alirekodiwa kwa video na kusambazwa kwenye mitandao ya kijamii.

Wakati kesi hiyo inasikilizwa, Mahakama hiyo ilikataa kupokea CD na picha kama kielelezo cha kesi hiyo kwa sababu upande wa Jamhuri ulishindwa kutimiza vigezo vya kisheria kuwasilisha vilelezo vya elektroniki mahakamani.

Wakili wa utetezi, Peter Kibatala, naye alipinga kupokewa kwa CD hiyo kwa madai kwamba shahidi aliyekuwa anawasilisha hakustahili kwani siye aliyeitengeneza CD hiyo.
Share:

Msomi ataka marekebisho ya sheria

MHADHIRI wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk James Jesse ameishauri Serikali kuwasilisha bungeni marekebisho ya Sheria ya Upigaji Kura ya Maoni ya Katiba Mpya ili kuendelea na mchakato wake kwani imepitwa na wakati.

Alitoa kauli hiyo jana Dar es Salaam wakati wa ufunguzi wa semina ya siku mbili ya Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kwa kushirikiana na Baraza la Uongozi la Dini na Amani (IRCPT) akisema marekebisho hayo yatafanya mchakato huo uende vizuri.

“Vifungu namba nne na tano vya hiyo sheria vinatakiwa kufanyiwa marekebisho ili mchakato uanze upya, vimepitwa na wakati,” alisema Dk Jesse.

Alisema maboresho hayo yanatakiwa kufanyika, kwani kwa sasa vifungu hivyo haviwezi kutumika kutokana na kwamba tarehe iliyopangwa kupiga kura ilishapita, kadhalika taratibu za kuendesha elimu ya mpiga kura haikufanyika.

Dk Jesse alieleza kuwa kutokana na hali hiyo inatakiwa kutangazwa upya tarehe ya kupiga kura ya maoni na kutoa muda kwa ajili ya elimu ya mpiga kura ili wanaounga mkono Katiba pendekezwa na wanaopinga waelimishwe juu ya wanachokiamini akisema baada ya hayo kufanyika ndipo kura ya maoni ifuate.

Alisema kutokana na kutoshiriki kikamilifu kwa wapinzani wakati wa kuijadili bungeni, Dk Jesse aliomba pia washirikishwe ili maoni yao mazuri yaongezwe kwa ajili ya kuiboresha Katiba hiyo.

Mkurugenzi, Utetezi na Maboresho wa LHRC, Anna Henga alisema lengo la semina hiyo ni kuwafundisha viongozi wa dini, ili waweze kushiriki kikamilifu katika suala la kurudisha mchakato wa Katiba Mpya.

“LHRC ina makubaliano na IRCPT kurudisha mchakato wa Katiba Mpya, tuna makubaliano ya kufundisha viongozi wa dini ili wachukue nafasi yao kwa ajili ya mchakato wa Katiba, ulianza na kuishia katikati,” alisema Henga.

Alisema wanataka mchakato urudi ambapo inatakiwa makundi yaweze kuchukua nafasi katika kuishauri Serikali.

Mkurugenzi wa IRCPT, Thomas Godda alisema anatamani kile ambacho kilianza kifikie tamati, kwani mchakato wa Katiba uligharimu fedha nyingi ambapo alieleza kuwa angefurahi kama Katiba ingekamilika kabla ya 2020.
Share:

ACT yalaani mpinzani kukamatwa Zambia

Zitto Zuberi Kabwe


CHAMA cha ACT-Wazalendo kimelaani Serikali ya Zambia kumkamata kiongozi wa chama kikuu cha upinzani cha United Party for National Development (UPND), Hakainde Hichilema ‘HH’ kwa madai ya uhaini.

Aidha, chama hicho kimesema vitendo vinavyofanywa na Serikali ya Zambia hasa kwa viongozi wa Upinzani ni ukiukwaji wa misingi ya demokrasia.

Taarifa hiyo ya kulaani ilitolewa jana na Katibu wa Mambo ya Nje wa ACT-Wazalendo, John Mbozu akibainisha kusikitishwa na vitendo vya ukamataji viongozi wa Upinzani katika nchi inayosimamia misingi ya demokrasia.

Alisema vitendo hivyo vinakwamisha juhudi za kukuza demokrasia katika bara la Afrika ambalo linapaswa kukubaliana na mabadiliko ya kidunia.

“Tumelazimika kusema haya kwa sababu matukio ya ukamataji viongozi wa vyama vya siasa vya upinzani unaonekana kuota mizizi na hii haikubaliki na Tanzania vitendo hivyo vipo pia,” alisema.

Alisema ACT-Wazalendo inaomba wapigania demokrasia, wanaharakati wa haki za binadamu, Umoja wa Afrika (AU) na Umoja wa Mataifa (UN) kuzungumzia suala hilo.

Alisema katika kupigania haki za binadamu na heshima ya mtu kokote duniani, chama hicho hakitarudi nyuma ili haki na usawa viweze kupatikana bila kuangalia dini, rangi na mipaka.

“Watu wote tunahitaji heshima na usawa kwa mujibu wa sheria kwa kufanya shughuli bila kuvunja sheria,” alisema.

Alisema Hichilema alishiriki uchaguzi mkuu wa Zambia dhidi ya Rais Edgar Lungu ambapo alimpa wakati mgumu.

Kwa mujibu wa Mbozu, Hichilema alikamatwa juzi usiku nyumbani kwake   New Kasama jijini Lusaka.

Alisema Hichilema atafikishwa mahakamani kwa tuhuma za uhaini na kwa mujibu wa sheria za Zambia, akipatikana na hatia atahukumiwa kunyongwa.

Aidha, inasemekana Hichilema hana rekodi yoyote ya makosa ya jinai na kwamba mashitaka hayo ni ya kutengenezwa ili kumaliza ndoto zake za kisiasa.
Share:
VITABU VYANGU
1. Hadaa: Unafiki Marekani, Ugaidi Duniani

2. Miaka 2000 ya Ukristo: Historia Iliyopotoshwa
Share:

Waliotembelea


Pekua blog hii

Definition List

© William Shao. Powered by Blogger.

Simple Post

Simple Post 2

New Carousel

Mag Post 2

Latest News

Most Recent

Latest Posts

2 Column Post

Mag Posts

Combined Post

Combined Posts 2

Video Posts

Follow us on facebook

Contact Form

Name

Email *

Message *

Contact Form

Name

Email *

Message *

Followers

Translate

About Sure Mag

Featured Videos

Put your ad code here

Popular Posts

Recent Posts

Unordered List

Theme Support

Unordered List